Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo, ametembelea banda la Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea katika Viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma, Juni 23, 2026. Katika ziara hiyo, Prof. Nombo alipata maelezo kuhusu huduma, programu na fursa mbalimbali zinazotolewa na TEWW kwa wananchi, pamoja na kujionea namna taasisi inavyotumia teknolojia na mifumo ya kidijitali katika kuboresha utoaji wa elimu nje ya mfumo rasmi.