Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga, Juni 6, 2026, ameshiriki katika Kongamano la Kijana na Malengo lililoandaliwa Ethics and Education Motivation Clubs (EEMC) chini ya Tanzania Youth Ministries (TAYOMI) katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), lililowakutanisha vijana kutoka vyuo mbalimbali vya mkoa wa Dar es Salaam kujadili masuala ya maadili, elimu, uongozi na maendeleo.
Katika kongamano hilo, Prof. Sanga ametoa mada kuhusu Uongozi unaosababisha matokeo, ambapo amesisitiza umuhimu wa uongozi unaomtanguliza Mungu, uwajibikaji na matumizi ya elimu katika kuleta mabadiliko chanya kwa jamii na Taifa.