Tarehe 8 Juni 2026, Prof. Philipo Sanga, Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), amefungua warsha ya ukatili wa kijinsia na rushwa kazini Dar es Salaam, akisisitiza umuhimu wa Dawati la Jinsia la TEWW kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu, weledi na usiri ili kujenga imani kwa wanajamii wa TEWW.
Mafunzo hayo yameendeshwa na wawezeshaji kutoka Jeshi la Polisi Makao Makuu pamoja na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU)