Mkuu wa TEWW, Prof. Philipo Sanga, akieleza shughuli za Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na mkakati wa kitaifa wa kisomo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mafunzo ya uendeshaji wa madarasa ya kisomo, Urambo - Tabora, Agosti 6, 2025
Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Dkt. Khamisi Mkanachi (katikati), akikabidhi vitendea kazi kwa Bi. Huruma Mgoo ambaye ni mwalimu wa kituo cha kisomo Urambo wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya uendeshaji wa madarasa ya kisomo Urambo – Tabora, Agosti 06, 2025. Huruma Daniel Mgoo
Mkuu wa Wilaya ya Urambo, Dkt. Khamisi Mkanachi (aliyeketi katikati), akifuatiwa na Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Prof. Philipo Sanga (kulia kwa mgeni rasmi), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanufaika wa madarasa ya kisomo mkoani Tabora baada ya tukio la uzinduzi wa mafunzo ya uendeshaji wa madarasa ya kisomo, Agosti 6, 2025, Urambo–Tabora.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda amesema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari leo Julai 17,2025 jijini Dodoma kuhusu maadhimisho hayo ambayo yanatarajiwa kufunguliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mnamo tarehe 25 Agosti,2025 na kufungwa Agosti 27,2025 na Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko.
"Maadhimisho haya yenye kauli mbiu isemayo: "Elimu bila ukomo kwa maendeleo endelevu" yanalenga kuhuisha kasi ya wadau wa kitaifa na kimataifa ya kuendeleza elimu ya watu wazima nchini na kuongeza uelewa wa umma kwamba elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi ni nyenzo muhimu kwa maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi", alisema Prof.Mkenda.
Amesema kuwa, maadhimisho hayo yanalenga kuangazia umuhimu mkubwa wa kujua kusoma na kuandika katika kuendelea kujifunza bila ukomo na kuamsha ari na hamasa miongoni mwa vijana na watu wazima ya kupata ujuzi katika masuala ya ujasiriamali na ufundi wa awali.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Hussein Omary, amesema kuwa mafunzo hayo ni kwa ajili ya kuwajengea uwezo Maafisa wa Magereza pamoja na wawezeshaji wa programu ya Kisomo yaliyofanyika jijini Dodoma.
Dkt.Omary amesema kuwa Tanzania, ambayo ilipiga hatua kubwa kufuta ujinga miaka ya 90, bado ina changamoto kubwa ambapo kwa mujibu wa sensa ya 2022, takribani asilimia 17 ya Watanzania hawana stadi za kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK).
“Mafunzo haya yanalenga kupunguza pengo hili na kuhakikisha kila Mtanzania anapata elimu na ujuzi wa maisha,” amesema.
Ameongeza kuwa Serikali imeanzisha vituo vya kisasa vya mafunzo na karakana za amali, sambamba na mbinu mpya ya RIFLEKTI inayochanganya elimu ya KKK na stadi za maisha ili kuwajengea wananchi uwezo wa kujitegemea kiuchumi.
Maadhimisho ya Miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima
Maadhimisho ya Miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima
DIRISHA LA UDAHILI LIMEFUNGULIWA 2025/2026
Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga amefanya ziara ya kikazi Mei 27, 2025 mkoani Tanga kujionea maendeleo ya karakana nne (4) zinazojengwa mkoani humo.
Katika ziara hiyo Prof. Sanga alitembelea karakana ya mfano inayojengwa Jijini Tanga na karakana nyingine za kawaida zinazojengwa Shule ya Msingi Magila (Halmashauri ya Muheza); Shule ya Msingi Ndeme (Halmashauri ya Lushoto); na Shule ya Msingi Makasini (Halmashauri ya Kilindi).
Ujenzi wa karakana hizo ni sehemu ya utekelezaji wa programu ya mpango changamani kwa vijana walio nje ya mfumo rasmi wa elimu (IPOSA) inayotekelezwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST) kupitia Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), kwa ufadhili wa Serikali ya Korea Kusini kupitia shirika la KOICA.
Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Prof. Philipo Sanga akipokea tuzo ya heshima kutoka kwa wawakilishi wa wahitimu wa Shahada ya Uzamili Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Machi 27, 2025 ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Wahitimu hao aliowahi kuwafundisha akiwa Mkufunzi chuoni hapo walitoa tuzo hiyo kutambua mchango wake katika kuendeleza elimu ya watu wazima nchini.
Prof. Philipo Lonati Sanga
Mkuu wa Taasisi
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (IAE) ilianzishwa mwaka 1960 kama kitengo cha masomo ya nje ya darasa cha Chuo cha Makerere, chini ya Chuo Kikuu cha London. Mnamo mwaka 1963, Taasisi hiyo iliboreshwa...