Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga (kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Korea Kusini, Mhe. Noel Kaganda (kulia), mara baada ya kumkabidhi zawadi za kumbukumbu, zikiwemo machapisho mbalimbali ya TEWW, wakati wa ziara ya heshima katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania nchini Korea Kusini.
CALL FOR BOOK CHAPTERS
DIRISHA LA UDAHILI
Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa DVV International Kanda ya Afrika Mashariki na Pembe ya Afrika, Frauke Heinze (kushoto), na Afisa Mwandamizi kutoka Makao Makuu ya shirika hilo nchini Ujerumani, Aminata Tamboura (kulia), baada ya mazungumzo ya kimkakati kuhusu kuimarisha elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi, Machi 2, 2026.
Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Philipo Sanga, akizindua rasmi mtaala mpya ulioboreshwa wa ABC Bible College & Training Center katika hafla iliyofanyika Kinyerezi, Dar es Salaam, tarehe 28 Februari 2026.
APPLY FOR THE CHINESE LANGUAGE SHORT COURSE
Mkuu wa Wilaya ya Babati, Bi. Emmanuela Kaganda (wa kwanza kushoto) na Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima, Prof. Philipo Sanga (wa pili kushoto) wakimsikiliza mmoja wa washiriki wa maonesho ya bidhaa bunifu zilizobuniwa na walimu wa Programu ya Elimu Changamani kwa Vijana walio nje ya Mfumo Rasmi wa Elimu (IPOSA), viongozi hao walipotembelea mabanda ya maonesho wakati wa kilele cha kuhitimisha mafunzo ya kuwajengea uwezo walimu wa programu ya IPOSA. Maonesho hayo ya siku moja yaliyofanyika mjini Babati Machi 14, 2025 yalizishirikisha halmashauri saba za Mkoa wa Manyara.
Mwenyekiti wa Baraza la Usimamizi la Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW), Prof. Zacharia Mganilwa (aliyekaa, kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza hilo mara baada ya kuhitimisha kikao chao cha kawaida makao makuu ya ofisi za TEWW jijini Dar es Salaam. Wa tatu (kutoka kushoto) ni Makamu Mwenyekiti wa Baraza, Dkt. Lulu Mahai, na aliyekaa (kulia) ni Katibu wa Baraza na Mkuu wa TEWW, Prof. Philipo Sanga.
Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (IAE) ilianzishwa mwaka 1960 kama kitengo cha masomo ya nje ya darasa cha Chuo cha Makerere, chini ya Chuo Kikuu cha London. Mnamo mwaka 1963, Taasisi hiyo iliboreshwa...